Nakumbuka zamani niliwahi kusoma kitabu cha hekaya
au ngano, vitabu ambavyo wengi tulivisoma bila kutafakari undani wake au maana
yake kiujumla.
Kuna simulizi hii ambayo naikumba mpaka leo na
nikifananisha na maisha haya ya sasa.
Kijana mmoja alikuwa anaishi na bibi/nyanya yake mzee, kwa
bahati mbaya alipokuwa amekwenda kucheza mbali na nyumbani kwao, uku nyuma Dubu
aliingia na kumla bibi/nyanya yake, kisha Dubu yule alilala na kujifanya kuwa ndio
bibi/nyanya ya yule kijana.
Yule kijana aliporudi mambo yalikuwa hivi:
Bibi mbona masikio yako makubwa?
Bibi akamjibu, ili niweze kukusikia vizuri.
Akamwuliza tena, mbona macho yako ni makubwa?
Akamjibu, ili niweze kukuona vizuri.
Akamwuliza, mbona meno yako makubwa?
Akamjibu, ili niweze kukutafuta vizuri.
Ndipo akaiona miguu yake na dubu yule akamrukia na
kumla...
Hiki ni kisa cha kutungwa hakina ukweli wowote
ndani yake, ni riwaya ambayo imeandikwa kwa niya ya kuburudisha na kufundisha
kidogo. Lakini tukichambua katika uono wa fasihi na kwa undani tunaweza
kuifananisha riwaya hii na maisha ya kisiasa.
Dubu huyu anaweza kuwa binadamu yoyote ambaye aidha
kwa njia moja ama nyingine tunamwamini, na kumuheshimu. Binadamu huyu ambaye
aidha tumempa madaraka au alikuja na kutuomba tumchaguwe ili awe ni mtetezi wetu
kwenye Nyanja za siasa na maisha kwa ujumla.
Nasi kwa kumuona kuwa ni mwenzetu na ni mwenye
kuonesha kuwa ana masikio makubwa ya kutusikia kilio chetu, na ana macho
makubwa ya kuona matatizo yetu, mdomo mkubwa wa kuyasemea matatizo yetu.
Lakini tumesahau kuwa Dubu huyu ana meno makubwa ya kutafuna mali asili zetu, kutafuna haki zetu, kutafuna kila anachokiona kuwa anaweza kukitafuna na kusahau kuwa kuna waliomchaguwa ili kusaidia kuwaletea maendeleo.
Lakini tumesahau kuwa Dubu huyu ana meno makubwa ya kutafuna mali asili zetu, kutafuna haki zetu, kutafuna kila anachokiona kuwa anaweza kukitafuna na kusahau kuwa kuna waliomchaguwa ili kusaidia kuwaletea maendeleo.
Matokeo yake kila kilicho kizuri si mali ya taifa tena,
bali ni mali binafsi za wanasiasa, wanasiasa ambao tumewapa dhamana ya kulinda
maliasili zetu, ili ziweze kutunufaisha sote, matokeo yake kumejengeka matabaka
makubwa kati ya wanasiasa na wale wanaoitwa walalahoi.
Hawa ni wananchi ambao vipato vyao havikizi hata
matumizi ya wiki moja, pale wanapopata pesa kichele, ambazo zinaitwa mshahara
wa kima cha chini.
Wananchi wanaweza kukubali kupokea kima cha chini
na wasilalamike pale tu watakapoweza kumuda maisha yao, watakapoweza kumudu
matibabu, kwenye hospitali zenye vifaa vizuri ambavyo mja mzito anaweza
kujifungua bila ya kutoa rushwa au kuja na pamba kutoka nyumbani kwake.
Mwananchi huyu anaweza asilalamike pale atakapoweza kusomesha watoto zao kwenye
shule ambazo walimu wanalipwa vema, ili waweze kufundisha vijana ambao
tunawaita ni taifa la kesho...!
Mwananchi anaweza asilalamike pale atakapoweza kula
na kunywa vyakula vyenye kuweza kurutubisha afya yake na kumtia nguvu
ya kuweza kwenda kuwajibika uko halipo ajiliwa au alipojihajili...!
Lakini haya yote yamekuwa ni ndoto za nchi ya kusadikika, kila kukicha hali inazidi kudorora, utapeli, wizi, ujambazi, umalaya, na halia ya kukata tamaa vinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Lakini haya yote yamekuwa ni ndoto za nchi ya kusadikika, kila kukicha hali inazidi kudorora, utapeli, wizi, ujambazi, umalaya, na halia ya kukata tamaa vinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Umefikia wakati sasa kwenye katiba ihainishwe wazi kabisa, kuwa kazi za siasa ndio kazi za wito, malipo yao yawe hayo ya kima cha chini maana wengi wa wanasiasa hatukuwatuma, bali walikuja wenyewe kututaka tuwachaguwe waende kutuwakilisha kwenye ilo linaloitwa Bunge la jamhuri ya muungano.
Kazi za ualimu, udaktari, uhuguzi, Polisi, Majeshi na zinginezo za
kuhudumia jamii si kazi za wito ni kazi ambazo wahusika wamezisomea na
kuzikeshea usiku ili kupata vyeti. Leo vipi hizo kazi ziwe ni wito, Fikra zangu
zinanambia kuwa kazi za Siasa ndio kazi za wito.
0 comments:
Post a Comment