Monday 15 June 2015


Habari zilizotufikia muda si mrefu ni kwamba Mufti Mkuu wa Tanzania Shekh Issa Shabani Simba Amefariki dunia, leo asubuhi.

Mufti Shekh Issa Shabani Simba, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Kisukari kwa muda mrefu kidogo.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, Mazishi ya Mufti Simba yatafanyika leo baada ya Swalat dhuhr shambani kwake uko Kigamboni.

Kwa wale wote watakaopata nafasi basi wanaweza kuudhuria Msibani nyumbani kwake Mikocheni, jijini Dar es Salaam.

--DUA'A
Ewe Mwenyezi Mungu  hakika Issa Shabani Simba yuko katika dhima yako na kamba ya ujirani wako, basi mkinge na fitina ya kaburi na adhabu ya moto nawe ndiwe mstahiki wa utekelezaji na ukweli, basi msamehe na umrehemu hakika Wewe ni mwingi wa kusamehe, mwingi wa kurehemu.

0 comments:

Post a Comment

99Graphix

99Graphix
99Graphix
Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!